Sunday, October 7, 2012

Reds Miss Tanzania watembelea kanda ya kaskazini

Warembo wakipata mlo wa mchana










JUMLA  ya warembo 29 kati ya 30 wanaowania taji la REDDS MISS TANZANIA 2012 leo wameanza ziara rasmi ya kutembelea Vivutio vya Utalii vilivyopo Kanda ya Kaskazini katika mikoa ya Moshi, Arusha na Manyara.
Warembo hao wakiongozwa na Viongozi wa Kamati ya Miss Tanzania, wakiwa katika mikoa hiyo watatembelea vivutio hivyo na kuhamasisha jamii ya watanzania kuwa na desturi ya kutembelea vivutio hivyo vyua ndani na kuhamasisha utalii. 
Pia warembo hao watapata fursa ya kujifunza vitu mbalimbali kuhusiana na masuala ya utalii. Oktoba 7, warembo hao watatembelea Hifadhi ya Mlima Kilimanjaro, katika lango kuu la kupandia Mlima huo la Marangu. 
Aidha kwa mujibu wa ratiba hiyo, inaonesha kuwa warembo hao watafanya tamasha la Michezo mjini Arusha kabla ya kuelekea Monduli ambako Oktoba 8 watazuru Kaburi la Waziri Mkuu wa Zamani, Hayati Edward Moringe Sokoine.

No comments:

Post a Comment

This is a public viewable website, post something that is not harmful to other people