Sunday, October 21, 2012

Spika wa Bunge Anne Makinda awasili Mjini Quebec, Canada kuhudhuria Mkutano wa 127 wa Chama cha Mabunge Duniani (IPU)

Afisa wa Ubalozi wa Tanzania nchini Canada Joseph Sokoine akimkabidhi Mhe. Spika taarifa ya maandalizi ya mkutano huo pamoja na hali ya kisiasa ilivyo nchini Canada baada ya kuwasili kuhudhuria Mkutano wa 127 wa Chama cha Mabunge Duniani (IPU).Picha na Owen Mwandumbya-BUNGE

  Spika wa  Bunge Mhe. Anne Makinda akiteta jambo kuhusu  maandalizi ya awali ya mkutano na afisa kutoka Bunge la Canada mara alipopokelewa baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege mjini Canada kuhudhuria mkutano wa 127 wa Chama cha Mabunge Duniani. Kulia ni Mhe. David Kafulila na Mhe. Hamad Rashid waliongozana na Mhe. Spika katika Mkutano huo nchini Canada

  Spika wa Bunge la Tanzania Mhe. Anne Makinda akiwasili katika uwanja wa ndege mjini Quebec, Canada tayari kwa kuhudhuria mkutano wa 127 wa chama cha Mabunge Duniani (IPU) unaotarajia kufunguliwa rasmi kesho tarehe 21 Oktoba, 2012 na kumalizika 26 Oktoba . Makinda ameongoja ujumbe wa wabunge wanne kutoka Tanzania, ambapo zaidi ya maspika wa nchi 150 duniani wakiongoza ujumbe wa wabunge kutoka Nchi zao watashiriki mkutano huo.






No comments:

Post a Comment

This is a public viewable website, post something that is not harmful to other people