Thursday, November 29, 2012

Kutoka Ofisi za Bunge:Rais Jakaya Kikwete Azindua Rasmi Ukumbi Mpya Wa Bunge la Afrika Jijini Arusha Leo


 Spika wa Bunge la Tanzania Mhe. Anne Makinda akimpokea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete wakati alipokuwa akiwasili katika jengo jipya la Jumuiya ya Afrika Mashariki Jijini Arusha kwa lengo la kuzindua Ukumbi wa Bunge la Afrika Mashariki ulioko katika jengo hilo.

Spika wa Bunge la Africa Mashariki Mhe. Margret Natongo Zziwa (kulia) akimkaribisha Spika wa Bunge la Tanzania Mhe. Anne Makinda katika jengo hilo leo.


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akilihutubia Bunge la Afrika Mashariki wakati alipofika kuzindua Ukumbi Mpya wa Bunge la Afrika Mashariki ulioko katika jengo jipya la Jumuiya ya Afrika Mashariki Jijini Arusha.

Jengo jipya la Jumuiya ya Afrika Mashariki.Picha na Prosper Minja- Bunge.

No comments:

Post a Comment

This is a public viewable website, post something that is not harmful to other people