Ndugu,nimekuwa
nikiandika kila mara ninapoona ujinga unaoenezwa juu ya
freemason.Ingawa binafsi nimekuwa nikikosoa namna watu wanavyobugizwa
propaganda zisizo na mashiko juu ya kuwa hiki ni kikundi cha waabudu
shetani na au wachawi,au kuwa wanauwezo wa kumfanya mtu tajiri,bado watu
wengi tu wamekuwa wakinipigia simu wakitaka niwasaidie kujiunga na
kikundi hicho.Nitumie fursa hii kusema tena kuwa mimi siyo tu siyo
mwanachama wa kikundi hicho,bali pia sifahamu namna kinavyopokea
wanachama wake.ninachojua na kwa uhakika kabisa sasa ni kuwa wajanja
wachache watawaibia wajinga hela zao kwa kuwaahidi uongo mtupu kama
kuwaingiza freemason ili watajirike.mfano tangazo hili juu nimelikuta
limebandikwa sinza,na namba za simu hizi zinapatikana,najaribu kuona
wanachoeleza hawa wapambe wa freemason wanaoweka matangazo.tujuavyo hata
kwa kusikia tu ni kuwa chama hiki kinasifika kwa kuwa chama cha
siri,nini kimetokea hapa tanzania mpaka kinaweka mabango kualika
wanachama? jibu ni rahisi,Tanzania ya siku hizi matapeli ni wengi.wapo
watakaotapeliwa kwa mtindo huu wa freemason.
Rwezahura
Rwezahura
No comments:
Post a Comment
This is a public viewable website, post something that is not harmful to other people