Thursday, November 1, 2012

Mwasiti asaini contract na Akon - Konvict

MSANII wa muziki wa Zouk mwenye sauti ya kiafrka zaidi Mwasiti, ameanza kutimiza ndoto zake kwani hivi karibuni amefanya kazi na producer wa msanii maarufu Akon, ngoma mbili ambazo ni ‘Woman’ na nyingine ambayo bado hajaipa jina kwani itakuwa ya kiswahili zaidi.

Producer huyo anafahamika kwa jina la Hakim, ndiye aliyeandika ngoma ya Akon ya ‘Mama Africa’ na kuiandaa katika studio za Konvict pamoja na ngoma nyingine kibao ambazo zimempa umaarufu.

Akiongea na DarTalk juu ya ishu hiyo aliposema kuwa producer huyo alikuwa nchini kwa wiki moja kwa ajili ya kutengeneza wimbo maalumu kwa ajili kombe la afrika, ndipo alipokutana naye ambapo alipata nafasi ya kuzisikiliza ngoma zake.

Msanii huyo alisema kuwa baada ya producer huyo kusikiliza ngoma zake akamuuliza swali kuwa anapenda kufanya naye swali ambao Mwasiti aliijibu kwa furaha kwani malengo yake anaamini sasa yanaenda kutimia.

Hata hivyo alisema ngoma hizo wamefanya na amezichukua kwa ajili ya kwenda kuzitengeneza na baada ya kukamilika atamtumia, ingawa anaamni ngoma yake moja ya ‘Woman’, itapigwa sana Afrika kwani amejaribu kuchangaya lugha mbili kiingereza na kiswahili.

“Yani kwanza siamini kupata bahati ya kukutana na producer mkubwa kamka huyo ambaye tayari ameshafanya kazi na wasanii wakubwa ambao wanatamba Afrika na Duniani, hivyo naamini malengo yangu yatatimia na kufika mbali kwa sababu mara kwa mara nazungumza na producer huyo na amekuwa akinipa moyo wa kufika,” alisema.

No comments:

Post a Comment

This is a public viewable website, post something that is not harmful to other people