Thursday, December 20, 2012

Hoteli za Double Tree by Hilton, Giraffe View zafungiwa kwa uchafuzi wa mazingira



Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Dkt. Terezya Huvisa (katikati) akitoa amri ya kuifunga hotel ya Double Tree kutokana na kutiririsha maji taka baharini. Wa kwanza kushoto ni Bw. Karim Kanji – Mkurugenzi Mkazi wa hotel hiyo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Dkt. Terezya Huvisa (wa kwanza kulia) akikagua mfumo wa maji taka katika Hotel ya Double Tree jijini Dar es Salaam. Kulia kwa Waziri ni Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais, Charles Kitwana na Dkt. Robert Ntakamulenga kutoka Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC).
Hotel ya Double tree iiliyofungiwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais – Mazingira, kutokana na kutiririsha maji taka baharini. Hotel hiyo imefungwa rasmi jana.

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEghrXEhH2Vm5KyIiTql4751G4LUSe8MblcbXYUDdgRn3Ffe0UGDHlnCJ4Yug8LnFp2wj255MVbuS2exHc3wGHBTlc0-FOpIGwLRHewxVP48tnQp1fVJCVQeja4kJMLBxIoB11hiZ0O320dN/s1600/_DSC0190.JPG
Waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu mazingira Dr. Terezya Huvisa akitoa amri ya kuifungia hoteli ya Giraffe ocean view iliyopo jijini Dar es Salaam alipozitembelea kukagua hali ya mazingira
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh9N5qY7jtoBl20mbkfpfCLjaHtjSXoC79Q1F0uUvGVqccE7RHSFe_qhyju-wASdIxOfbLgCA6LHkn5Fs8sRcgXEkGZ_-S9VX0l-qW2ACcH5kYR9S98DL4Y6zT4amzWP_BDBZNSTY0lnPz1/s1600/_DSC0109.JPG 

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh6gPu9jrEgPdZA5ARQ_ya-wBULPfrYfK2U2jzUrw5CZCvt_Z9Oj0SKIFYccJTgxkPkBOb_U_x6j7IugY9baZYf-VZMHngT2m520zsWeWhqKBXA_WUKmHHk27gNhxJ3I7mb8DgzSFnxZ2d1/s1600/_DSC0098.JPG 
Na Lulu Mussa na Ali Meja
Waziri wa Nchi wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais – Mazingira Dk. Terezya Huvisa hii leo ameifungia hotel ya Double Tree na Giraffe Ocean view za Jijini Dar es Salaam kutokana na kutiririsha maji taka baharini.
Waziri Huvisa ametoa agizo hilo mara baada ya kufanya ziara ya kushtukiza akiwa na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mheshimiwa Charles Kitwanga. 
Ziara hiyo ililenga kuona utekelezaji wa maagizo yaliyotolewa awali na Naibu Waziri Mh. Charles Kitwanga mapema mwezi huu, alipofanya ziara kutembelea viwanda na hoteli zilizo pembezoni mwa bahari kuona mfumo wa maji taka. 
Katika ziara hiyo, Hotel ya Double Tree iliagizwa kuwa na mpango wa muda mfupi na wa haraka wa kusitisha utiririshaji wa maji taka baharini ambao mpaka leo hotel hiyo ilikuwa bado haijatekeleza. 
Sambamba na hilo na hilo Waziri Huvisa amefuta hati ya ukaguzi wa Mazingira (Environemental Audit) na kuitaka hoteli hiyo kurekebisha mara moja mfumo huo ikiwa ni sambamba na kulipa faini kwa baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC).

No comments:

Post a Comment

This is a public viewable website, post something that is not harmful to other people