SERIKALI imewataka wote waliokopeshwa kwa ajili ya kusoma elimu
ya juu nchini kuirejesha kwa hiari mikopo hiyo kwa Bodi ya Mikopo ya
Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HELSB) na wasipofanya hivyo watafuatiliwa na
wakala maalumu aliyeajiriwa na bodi hiyo kwa ajili ya kuwafuatilia ambao
hawajairejesha mpaka sasa.
Imesema mpaka kufika Septemba mwaka huu fedha
zilizokusanywa ni Sh23.3 bilioni kutoka kwa watu 48,235 na kwamba
kiwango hicho ni chini ya asilimia 50 ya fedha zilizotakiwa kurudishwa,
chini ya asilimia 50 ya watu wanaotakiwa kurejesha mikopo hiyo.
Akizungumza katika kipindi cha dakika 45
kinachorushwa na Televisheni ya ITV, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya
Ufundi , Dk Shukuru Kawambwa alisema suala la urejeshwaji wa mikopo bado
ni changamoto kubwa.
“Hawa 48,235 ni wale ambao bodi imewagundua wako
wapi na wanafanya kazi gani, wengine hawajagundulika wako wapi hata
hawajitokezi sijui wanataka mpaka watafutwe,” alisema Kawambwa na
kuongeza:
“Bodi imeajiri wakala maalumu kwa ajili ya kuwafuatilia watu ambao hawajarejesha mikopo, lengo ni kuhakikisha fedha hizi zinakusanywa ili kuwasaidia wanafunzi wengine.
“Bodi imeajiri wakala maalumu kwa ajili ya kuwafuatilia watu ambao hawajarejesha mikopo, lengo ni kuhakikisha fedha hizi zinakusanywa ili kuwasaidia wanafunzi wengine.
“Nimeiambia bodi kuwa, hatuwezi kuzungumza vizuri
kabla ya kufanya kazi nzuri ya kurejesha mikopo, nimewaeleza wazi kwamba
hawawezi kutoa mikopo wakati hawairejeshi ipasavyo, sasa hakuna kulala
ni kazi tu,” alisema Kawambwa.
Alifafanua, “Kama waliotakiwa kurejesha mikopo
wangefanya hivyo kwa wakati ni wazi kuwa idadi ya wanafunzi watakaopata
mikopo ingeongezeka kwa kiasi kikubwa, lengo la Serikali ya awamu ya
nne ni kuona kila mwanafunzi anapata mkopo.”
Alisema mwaka 2004-2005 wanafunzi 6,000 tu ndiyo
waliopewa mikopo na kwamba mwaka huu idadi hiyo imeongezeka hadi
kufikia wanafunzi 98,000.
Alifafanua Mwaka 2004 -2005 fedha iliyotolewa kwa ajili ya mikopo ni Sh9.9 bilioni na kwamba bajeti ya mwaka huu ni Sh326 bilioni.
Alifafanua Mwaka 2004 -2005 fedha iliyotolewa kwa ajili ya mikopo ni Sh9.9 bilioni na kwamba bajeti ya mwaka huu ni Sh326 bilioni.
Akizungumzia wanafunzi wanaostahili kupewa mikopo,
Dk Kawambwa alisema kila mwaka taratibu za mikopo zinafanyiwa
marekebisho ili ziwe na manufaa zaidi na kwamba hilo limetokana na
ushauri mbalimbali kutoka kwa wadau wa elimu nchini.
“Kwanza huwa wanatizamwa wanafunzi waliofanya
vizuri katika mitihani yao kwa kuwa Serikali ya Tanzania imeamua
kuwekeza kwa wanafunzi waliofaulu vizuri zaidi,” alisema Kawamba na
kuongeza:
“Lakini baada ya kusikiliza ushauri tulianza kutizama uhitaji zaidi, sasa tunaangalia anayeomba mkopo anahitaji kweli kupewa, pia tunatizama vipaumbele tulivyojiwekea ambavyo ni wanafunzi wanaosomea udaktari, ualimu na uhandisi.”
Alisema kutokana na hali hiyo mwaka huu asilimia 50 ya wanafunzi walioomba mikopo ni walimu.
“Lakini baada ya kusikiliza ushauri tulianza kutizama uhitaji zaidi, sasa tunaangalia anayeomba mkopo anahitaji kweli kupewa, pia tunatizama vipaumbele tulivyojiwekea ambavyo ni wanafunzi wanaosomea udaktari, ualimu na uhandisi.”
Alisema kutokana na hali hiyo mwaka huu asilimia 50 ya wanafunzi walioomba mikopo ni walimu.
“Walimu kujiendelea kielimu ni jambo zuri lakini
sio kukimbia kufundisha kwa lengo la kusoma, tumewaruhusu baadhi ya
walimu kusoma na wengine tutawaruhusu mwakani” alisema Kawambwa.
Akizungumzia suala la wanafunzi kufanyiwa udahili
mara mbili, alisema Tume ya Vyuo Vikuu (TCU) imeanzisha mpango wa awamu
ya pili ya kudahili wanafunzi unaoitwa, Mpango wa Pamoja wa Kudahili
Wanafunzi (CAS) na kwamba umetengenezwa kwa teknolojia ya hali ya juu.
“Wanafunzi walioomba nafasi sasa wanaingizwa
katika mfumo huo na kuchambuliwa kulingana na sifa zao hakuna
atakayependelewa, kila mwenye sifa atapangiwa fani atatakayosoma”
alisema Kawambwa na kuongeza:
No comments:
Post a Comment
This is a public viewable website, post something that is not harmful to other people